Quantcast
Channel: Www.maxwellyblogspot.com
Viewing all 3608 articles
Browse latest View live

Stori ya Mzee wa miaka 80 mwenye Watoto 100 na bado anahitaji wengine.

$
0
0
Bilashaka moja kati ya stori inayoendelea kuwaacha watu wengi midomo wazi ni hii ya Mzeze mwenye umri wa miaka 80, Kofi Asilenu raia wa Ghana ambaye ana watoto 100 amedai bado anahitaji kuongeza watoto wawili katika familia yake.

Asilenu ana wake 12 na anaishi na familia yake katika kijiji cha Amankrom kilicho umbali wa kilomita 45 kutoka mji mkuu wa nchii hiyo, Acca. 
Familia yake ni thuluthi moja ya watu 600 katika kijiji anachoishi.

Sababu ya yeye kutaka kuendelea kuzaa ameeleza kuwa anahitaji familia kubwa kwa sababu hapo awali hakuwa na ndugu, “sina kaka wala shangazi, ndio sababu niliamua kuwa na watoto wengi ili nipate maziko mazuri nikifa,” alisema Asilenu.

Picha:Beyonce aonyesha picha ya watoto wake mapacha kwa mara ya kwanza.

$
0
0

A post shared by Beyoncé (@beyonce) on
Dunia imekuwa ikisubiria kwa hamu kuona watoto wa mapacha wawili wa mastaa Beyonce (35) na Jay Z (47), ambapo leo Ijumaa Queen Bey amevunja ukimia kupitia account yake ya Instagram na kuweka picha yake akiwa amebeba mapacha wao.

Kati ya mastaa walio like picha hiyo ni pamoja na Kim Kardashian, ambae familia yake kwa siku za usoni hawakuwa na mahusiano mazuri.

Priyanka Chopra star wa filamu za Kihindi ameungana na mkali kutoka Hollywood.

$
0
0
Moja kati ya stori kama wewe ni shabiki wa filamu za Kihindi, hii ya staa wa filamu kutoka katika kiwanda cha filamu Bollywood India, Priyanka Chopra baada ya picha hizi na kipande cha video kuvuja akionekana Location "New York City’s Central Park" nchini Marekani na staa wa Hollywood.
Wiki hii Staa Priyanka Chopra amekuwa location akishuti filamu yake mpya kutoka Hollywood inayoitwa "Isn’t It Romantic"? aliyomshirikisha staa wa hollywood Adam DeVine, picha unazoziona hapo niwakati wakiwa katika uigizaji.

Sasa chungulia hapo video iliyosemekana kuvuja wakati wanaigiza video hiyo>>>

Movie mpya ya Sidharth Malhotra na Jacqueline Fernandez inayoitwa 'Gentelemen' kutikisa.

$
0
0
Hii inakuwa mara ya kwanza kwa mwanadada Jacqueline Fernandez na mkali Sidharth Malhotra kuigiza pamoja katika movie hii inayokwenda kwa jina la Gentlemen inayotarajiwa kuachiwa rasmi mwezi August 25th, 2017.

Sasa kama wewe ni shabiki wa movie za Kihindi, huu ndio mtonyo ambao unapaswa kuufahamu wakwetu, ambapo hiyo hapo juu ndio poster official ya Gentlemen.

Ujio wa Sanjay Dutty 'Star wa filamu za Kihindi' umekuwa gumzo Tanzania.

$
0
0
Magazeti, Redio, Tv na mitandao ya kijamii vimeonekana kumzungumzia muigizaji mkongwe na  anayefanya vizuri kwenye soko la filamu India, Sanjay Balraj Dutt, aliyekuja nchini kwa ajili ya mapumziko anatarajiwa kudumu kwa siku 21 ambapo atatembelea mbuga za wanyama na vivutio mbali mbali vilivyopo nchini. 

Ujio wa Sanjay Dutt umethibitishwa na mwenyeji wake ambaye ni Mbunge wa Manonga, Seif Gulamali ambaye amesema uwepo wa msanii huyo ni kipimo cha kuwa sekta ya utalii nchini inaendelea kupanuka.
Muigizaji Sanjay Dutt (kushoto) akipeana mkono na Mbunge Gulamali
"Uwepo wa Sanjay Dutt nchini ni fursa kubwa sana.Wahusika wa utalii hapa nchini wakiona fursa katika kuutangaza zaidi utalii wetu ni vyema pia wakamtumia kwani mtu huyu ni mkubwa sana kwenye sanaa ya filamu. 

Lakini pia kuja kwake hapa nchini ni wazi tunazidi kukua kwenye sekta hii, na tutapata mapato kupitia kuwepo kwake kwani atakuwepo kwa takribani siku 21" alisema Mhe. Gulamali
Hata hivyo mbunge huyo amewataka waigizaji wa filamu nchini kuchangamkia fursa ya kukutana na muigizaji huyo kwa ajili ya kupata madini yatakayowasaidia kukuza na kupanua soko la filamu.

Sanjay Dutt amefika Arusha mapema jana akitokea Dar es salaam kwa ajili ya kuzuru mbuga za wanyama, Ngorongoro, Serengeti, mbuga ya Selou na vivutio vingine vilivyopo nchini.
Chanzo: Eatv

Asili Yetu Tanzania inakuletea punguzo maalum la msimu wa Nane Nane 2017 kwa kutangaza shughuli yako kwa bei nafuu.

$
0
0
Asili Yetu Tanzania Blog kupitia kurasa zake za mitandao ya habari online, inapenda kukutaarifu ewe mkulima, mjasilia mali na mtu yeyote unayehita shughuli yako ifahamike na mamilioni ya watukupitia mitandao yetu online (Asili Promo), unakaribishwa kuchangamkia ofa hii maalu.

Kutokana kuwa tunauzalendo na nchi yetu Tanzania, basi ASILI YETU TANZANIA BLOG kupitia kitengo chake cha promotion (Asili Promo) imetoa punguzo maalum la kutangaza shughuli yako katika msimu huu wa sikukuu ya wakulima NANE NANE.

Ziko ofa nyingine nyingi utakazozipata (mteja wetu) endapo utatangaza nasi, aidha kwa kupost habari yako katika mtandao wetu au kuweka tangazo asilia, litakaloonekanakwa mamilioni wa folower wetu.

Kwa mawasiliano zaidi tumia hizo namba hapo juu kwenye banner.

Mfuko wenye vumbi na mawe kutoka Mwezini wapigwa mnada Marekani.

$
0
0
Mfuko moja uliotumika na mwananga Neil Amstrong kukusanya violezi vya mwezi, umeuzwa kwa dola milioni 1.8 mjini New York.
 
Mfuko huo katika chombo cha angani cha Apolo 11 mwaka 1969 ulinunuliwa katika eneo la Sotheyby na mtu asiyejulikana.
 
Mfuko huo bado una vumbi na mawe madogo madogo kutoka mwezini.
 
Mnada huo unajiri baada ya mapambano mahakamani kuhusu umiliki wa kifaa hicho cha kipekee kutoka Apollo 11 ambao ulikuwa katika mikono ya mtu binafsi.
 
Baada ya chombo hicho cha angani kurudi duniani, vifaa vyote vilipelekwa katika jumba la makumbusho la Smithsonian.
 
Hatahivyo mfuko huo uliachwa katika boksi katika kituo cha vyombo vya angani cha Johnson kutokana na makosa ya kihesabu.
 
Baadaye haukutambulika wakati wa mnada wa serikali, ukiuzwa kwa dola 995 pekee kwa wakili mmoja wa Illinois 2015.
 
Hatahivyo mamlaka inayosimamia vyombo vya angani Nasa ilijarabu kuuchukua mfuko huo, lakini mapema mwaka huu, jaji mmoja aliamuru kwamba, ulimilikiwa na mnunuzi huyo kimakosa ambaye baadaye ailiupeleka katika mnada huo wa Sutheby.
Chanzo: BBC

Tanzania yatajwa kama kivutio bora cha Utalii kwa mwaka 2017

$
0
0
Tanzania imetajwa kuwa kivutio kizuri cha safari za watalii barani Afrika kulingana na mtandao wa SafaricBookings.com ambao ndio mtandao mkubwa wa ukuzaji wa safari za Afrika.

Mtandao huo ulifanya tathmini ya zaidi ya wataalam 2500 na wale walioshiriki katika safari hizo kabla ya kutangaza kuwa Tanzania ndio eneo bora la safari mwaka 2017.

Tathmini hizo ziliandikwa na watalii walioenda safari pamoja na wataalam bingwa wa Afrika.

Mtandao huo unasema kuwa, uchanganuzi huo pia ulibaini kwamba Tanzania ilipata umaarufu wake kutokana na idadi ya wanyama mbali mbali.
Watu maarufu katika miezi ya hivi karibuni wamekuwa wakizuru Tanzania, kwa kwakutembelea maeneo tofauti ya vivutio vya utalii nchini Tanzania.

Watu hao ni mwanamuziki maarufu Usher Raymond, aliyekuwa mchezaji wa klabu ya Manchester United na Real MadridDavid Beckham, aliyekuwa mchezaji wa Liverpool Mamadou Sakho, mchezaji wa EvertonMorgan Schneiderlin na nyota wa filamu kutoka Marekani Will Smith na Harrison Ford.

Walitembelea mbuga za Serengeti na mlima kilimanjaro.
Mtandao huo uliitaja Zambia kuwa taifa lenye kivutio kizuri cha misitu huku wataalam wote wakikubaliana kwamba mazingira ya
misitu nchini humo mi mazuri zaidi.

Vilevile Zambia pia ilitajwa kuwa taifa lenye maisha bora ya ndege.
Namibia na Kenya zilitajwa kuwa bora katika mandhari mazuri pamoja na ndege waliopo mtawalia.

Chanzo:BBC

Tiketi za kushuhudia pambano la ngumi kati ya Mayweather na McGregor za weka rekodi.

$
0
0
Tiketi za kushuhudia mpambano wa masumbwi kati ya Floyd Mayweather dhidi ya Conor McGregor zinauzwa kwa dola 150,000.
Mpambano huo unatajwa kuwa wa gharama zaidi kuwahi kutokea na tiketi kwa sasa zinauzwa kama njugu.

Unatarajiwa kupigwa Agosti 26 katika uwanja wa T-Mobile mjini Las Vegas utakaoingiza watu elfu 20.

Mayweather mwenye miaka 40 awali alistaafu mchezo wa masumbwi lakini amerejea tena kupambana na McGregor.

Video: Harmonize - 'Sina'

$
0
0
Msanii kutoka Wasafi Classic Baby maarufu kama Harmonize baada ya kuwa na collable kibao kupitia ngoma zake na nyingine alizoshirikishwa na wasanii wenzake, sasa ameachia video Mpya wa waimbo wake wa 'SINA'.

Katika video hii mkongwe wa TAKEU STYLE Mr. Nice ameonekana.

Utazame hapo chini>>>

Tajiri namba 1 duniani kwa mwaka 2017 ni Jeff Bezos ampiku Bill Gates.

$
0
0
Mwanzilishi wa Kampuni ya Amazon, Jeff Bezos amempita Bill Gates na kuwa tajiri namba moja duniani akimiliki utajiri wa dola za kimarekani 90.6 bilioni (Tsh 203 trilioni).

Kupanda kwa hisa za Amazon kwa asilimia 1.5 Julai 27 kulimaanisha kuwa tajiri huyo amempita mwanzilishi mwenza wa Microsoft, kwa mujibu wa taarifa za jarida la Forbes la nchini Marekani.

Forbes wameeleza kuwa Bezos ana utajiri wa $90.6 bilioni akimzidi Bill Gates aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo akiwa na utajiri wa $90 billioni sawa na Tsh 201.5 trilioni.

Bezos ananakadiriwa kumilikia hisa milioni 80 za Amazon akiwa ni mwenye hisa nyingi zaidi ya mwingine yeyote.

Kwa miaka ya hivi karibuni amekuwa akijikita zaidi katika mradi wake wa Blue Origin unaohusika na urushaji wa rocket kwenda angani pamoja na Washington Post ambazo zote anazimiliki.

Bezos ambaye ni Mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji Mkuu (CEO) wa Amazon alizaliwa mwaka 1964 Albuquerque Jimbo la New Mexico na alisoma Sayansi ya Kompyuta na Uhandisi wa Umeme katika Chuo Kikuu cha Princeton.

Alipohitimu alikwenda kufanya kazi na Wall Street lakini mwaka 1994 aliacha kazi na kwenda kuanzisha Amazon ambapo kwa mara ya kwanza Amazon ilianzishiwa katika karakana ya kutengenezea magari. 

Baada ya kampuni hiyo kuanza kufanikiwa na kujipanua katika nchi mbalimbali, mwaka 2000 alianzisha kampuni ya Blue Origin inayojishughulisha na masuala ya anga.

Mwaka 2013 akiendelea kujipanua, aliinunua Kampuni ya Washington Post kwa dola milioni 250  na ilipofika Mei 2017 alitajwa kuwa na utajiri wa dola bilioni 84.8 , lakini leo Julai 27, 2017 amefikisha utajiri wa dola bilioni 90.6  na kushikilia usukani wa mtu tajiri zaidi duniani.

Kwa mujibu wa Forbes, hawa ndio matajiri 10 wanaoongoza duniani;

  1. Jeff Bezos (53)- Amazon.com
  2. Bill Gates (61)- Microsoft
  3. Amancio Ortega (81)- Zara
  4. Warren Buffett (86)- Berkshire Hathaway
  5. Mack Zuckerberg (33)- Facebook
  6. Carlos Helu (77)- telecom
  7. Larry Ellison (72)- software
  8. Michael Bloomberg (75)- Bloomberg LP
  9. Bernard Arnault (68)- LVMH
  10. Charles Koch (81)- diversified

Mtandao wa WhatsApp unaongoza kwa kuwa na watumiaji wengi kila siku

$
0
0
Mtandao wa kijamii wa WhatsApp umebainika kutumiwa na watu Bilioni moja kwa kila siku.

Mnamo mwaka jana mtandao huo ulikuwa na watumiaji bilioni moja ila sasa idadi hiyo imekuwa ni ya wanaotembelea kila siku, inadaiwa kuwa katika watu kumi kati ya watu wanane hadi saba wanatumia mtandao huo. 

Mitandao mingine inayoongoza kuwa na watumiaji wemngi kwa siku ni Facebook , Instagram na Messenger.

Utafiti uliofanyika mwaka 2014 na Chuo Kikuu cha Pittsburgh cha Pennsylvania nchini Marekani, ulibaini  kuwa alisimia 71 ya wanotumia mitando ya kijamii  ni vijana na hutumia kila baada ya dakika 10.

Rais mstaafu Dkt Jakaya Kikwete ni mkulima mzuri wa kuigwa.

$
0
0
Rais Mstaafu Jakaya Kikwete amezidi kuonyesha mfano katika kilimo baada ya kuonekana akiwa katika mashamba yake ya Mizabibu Dodoma
Kupitia mtandao wa twitter Mh. Kikweteameandika,Nikiwa Dodoma nimepata wasaa wa kutembelea na kukagua shamba langu la mizabibu. Mwaka huu mavuno yatakuwa mazuri Insha Allah.
June 4mwaka huu  pia alifanya hivyo kwa kuandika,Kuna maisha baada ya Urais hususani wasaa wa kufanya yale uliyokosa muda wa kuyafanya kama kutumia muda na familia,kuangalia mifugo na shamba”. 

 Kisha kuweka picha akiwa katika shamba lake la mahindi kijijini Msoga.

Aamir Khnan ahamasisha watu kujitolea kuwasaidia watu walioathiriwa na mafuriko Gujarat India

$
0
0
Hali  ya maeneo ya Gujarat nchini India sio nzuri, ikiwa ni baada ya hivi karibuni kukumbwa na mafuriko makubwa, yaliyosababisha kupoteza maisha ya takribani watu 120 na hasara mbali mbali.
Pamoja na mafuriko ya hivi karibuni yaliyotokea, serikali imekuwa na hasara kubwa. Superstar Aamir Khan amechukua time kupitia ukurasa wake wa Twitter kuonesha huzuni yake juu ya kupoteza maisha na makazi ya watu.

Katika video aliyoiweka Twitter Aamir ameonekana akiwahamasisha watu kuchukua hatua ya kuwasaidia wakazi wa Gujarat ambao takribani 10,000 kutoka maeneo ya vijijini na mijini wamekosa sehemu ya kuishi.
Aamir anajulikana kwa huduma zake za kijamii na kuwakumbusha watu wajibu wao, kwa wananchi wenzake. 

Katika siku za nyuma pia, amewahi kujitoa kuhamasisha watu kujitoa katika kuisaidia jamii.
Hii pia ni hatua muhimu sana iliyochukuliwa na Aamir ili kuwasaidia watu wa Gujarat.

 Star huyu hivi karibuni ataonekana katika movie mpya ya Secret of Superstar, iliyopangwa kuachiwa mwezi Oktoba

Mbali na hilo, sasa anafanya kazi kwenye katika filamu ya Thug of Hindostan na star Amitabh Bachchan, Fatima Sana Shaikh na Katrina Kaif.

Salman Khan ataperfom kwenye tuzo za Big Zee Entertainment 2017

$
0
0
Kwa stori zilizovuja hadi sasa, ni kuhusuBollywood Super Star Salman Khan kuperfome katika BIG Zee Entertainment Awards 2017.
 Mkali wa Sultan, Salman Khan atapanda stage na kufanya shoo katika Tuzo za Big Zee Entertainment
 
Ambapo chanzo kinasema kuwa Salman ataonyesha shoo katika awamu tatu na huku ya tatu ikionesha upande wake wa pekee kwa watazamaji katika sehemu ya mwisho, katika tuzo hizo.
Tuzo hizo zitashereheshwa na mwandaaji wa filamu Karan Johar na mwigizaji-mchekeshaji Sunil Grover.

BIG Zee Entertainment Awards 2017 itaoneshwa kwenye TV live tarehe 13 Agosti 2017.

Uzinduzi wa Usharika Mpya wa Ilkiranyi (KKKT) wafana Jijini Arusha

$
0
0
July 30 2017 Jijini Arusha viongozi wa dini wakiongozwa na Baba Askofu Dkt Solomon J Masangwa pamoja na wageni waalikwa na baadhi ya viongozi wa Serikali, walijumuika katika Ibada ya Uzinduzi na uwekaji wa jiwe la msingi katika Usharika Mpya wa ILKIRANYI.

Hayo yalifanyika jana katika kanisa la KKKT Dayosisi ya Kaskazini Kati Jimbo la Arusha Magharibi katika Usharika Mpya wa ILKIRANYI ambapo baadhi ya viongozi waliyohudhuria ni pamoja na Mbunge wa Jimbo la Arumeru mh. Gibson Meseyek, Meya wa Jiji la Arusha Kalist Lazaro na wengineo.

Tazama video hapo chini, uone jinsi ilivyokuwa>>>
Gibson Meseyek Mbunge wa jimbo la arumeru akitoa shukran zake kwenye ibada ya uzinduzi wa usharika wa Ilkiranyi>>> Kalist Lazaro Maya wa jiji la arusha akitoa shukran kwenye ibada ya uzinduz wa usharika wa ilkiranyi>>>

Sayansi na Teknolojia: Binadamu wazalisha tani bilioni 8.3 za plastiki duniani

$
0
0
Utafiti mpya uliotolewa kwenye gazeti la Science Advances unasema, tangu mwanzoni mwa miaka ya 50 karne iliyopita, binadamu wamezalisha tani bilioni 8.3 za plastiki, ambazo nyingi zimekuwa takataka.

Kikundi cha watafiti kutoka Chuo Kikuu cha Georgia, tawi la St. Barbara la Chuo Kikuu cha California, na taasisi ya elimu kuhusu bahari, wamefanya utafiti kuhusu uzalishaji, matumizi ya plastiki na takataka za plastiki, wamegundua kuwa, mwaka 1950 uzalishaji wa plastiki duniani ulikuwa tani milioni 2, na ifikapo mwaka 2015, uzalishaji huo ulifikia tani milioni 400, ambao ni mkubwa zaidi kuliko vitu vingine, isipokuwa saruji na chuma. 

Miongoni mwa tani bilioni 8.3 za plastiki zilizozalishwa, tani bilioni 6.3 zimekuwa takataka. 

Na miongoni mwa takataka hizi, asilimia 9 tu zimerudishwa viwandani ili kutumiwa tena, asilimia 12 zimeteketezwa, nyingine asilimia 79 zimezikwa ardhini au kuachiwa katika mazingira yetu.
Kwa mujibu wa mwelekeo wa sasa, ifikapo mwaka 2050, kutakuwa na tani bilioni 12 za takataka za plastiki duniani.



Plastiki nyingi haziwezi kuoza ndani ya muda mfupi, zitakuwepo kwa mamia hata maelfu ya miaka.


 Mwaka 2010 tani milioni 8 za plastiki ziliingia baharini.
Watafiti wamesema binadamu wanatakiwa kufikiri suala la kushughulikia takataka na kudhibiti matumizi ya plastiki kwa makini zaidi.
Chanzo: CRI

VIDEO: Mr Blue Ft. JR - "Siwezi".

$
0
0
Baada ya staa kutoka BongoflevaniMr. Blue a.k.a Byser auBabylon Bizz kuiachia single yake mpya “Siwezi” iliyotayarishwa na Man Walter kutoka Combination Sound, tayari ameifanyia video na nimekuwekea hapo chini>>>

Daraja linalokisiwa kuwa refu zaidi duniani lazinduliwa nchini Uswizi

$
0
0
Daraja lililotundikwa lenye mita 500 linalokisiwa kuwa refu zaidi duniani limefunguliwa katika mji wa Zermatt nchini Uswizi.

Daraja hilo lenye urefu wa mita 494 kwa jina Europabrucke limetundikwa mita 85 juu.
Bodi za utalii ya Zermatt inasema kuwa ndio daraja refu zaidi duniani ,ijapokuwa daraja la mita 405 mjini Reutte Austria limetundikwa mita 110 juu kutoka ardhini.

Daraja hilo linachukua mahala pa daraja jingine ambalo lilikuwa limeharibiwa na mwamba.
Daraja hilo jipya ambalo ambalo lina uzito wa tani nane limewekwa kifaa cha ambacho linalizuia kuyumbayumba ,kulingana na bodi ya watalii ya Zermatt.

Daraja hilo lipo kati ya Zermatt na Grachen kusini mwa Switzerland.
Stori na BBC

Anushka Sharma ndani ya filamu moja mpya na Shah Rukh Khan

$
0
0
Moja kati ya combination ambayo imekuwa ikiwavutia sana mashabiki wa filamu za kihindi sehemu nyingi duniani, ni hii ya Malikia wa Filamu Bollywood Anushka Sharma na SuperstarShah Rukh Khan - SRK kuonekana katika filamu moja.
Kwa historia iliyopo katika wakali hawa wawili katika movie walizowahi kukutana pamoja, imekuwa ni amazing, kwamfano movie ya Rab Ne Bana Di Jodi (2008), Jab Tak Hai Jaan (2012), Ae Dil Hai Mushkil (2016), zote hizi zilionekana kuwa na matunda japo ni zakushirikishwa kwa wakali hawa.
 Sasa safari hii baada ya mkali SRK kuachia filamu yake Raees mwezi Januari na kufanya vizuri, sasa ile combination inajirudia, namzungumzia Shah Rukh Khan na Anushka Sharma.
Agosti 4, 2017 mkali Shah Rukh Khan akimshirikisha mwanadada  Anushka Sharma ataachia filamu mpya inayokwenda kwa jina'Jab Harry Met Sejal', nimatumaini yetu tunaisubiri kwa hamu kuona utamu wake kati ya hawa masuperstar.

Karibu ujiunge na blog yetu ya Asili Yetu Tanzania kwa update zaidi.
Viewing all 3608 articles
Browse latest View live




Latest Images